BUCHAMBI, NG'WANIMA ZANG'ARA BONANZA LA MICHEZO MONDO- KISHAPU

Shule za msingi na sekondari Tarafa ya Mondo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga zimekutana katika bonanza la michezo lililolenga kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji vya wanafunzi, hususan mchezo wa netiboli katika ngazi za shule za msingi na sekondari Julai 31, 2026 viwanja vya michezo shule ya Msingi Ng'wanima lililoandaliwa na Walimu wa michezo wa shule hizo.


Bonanza hilo lilihusisha michezo ya mpira wa Pete na mpira wa miguu, huku shule mbalimbali zikishindana kuonesha uwezo wao. Katika mchezo wa pete, Shule ya Msingi Buchambi imeibuka mshindi, wakati Shule ya Msingi Ng’wanima ikitwaa ubingwa wa mpira wa miguu.


Bonanza hilo limeshirikisha jumla ya shule nane ambazo ni Ng’wanima Primary, Busangwa Primary, Ng’wajipugila Primary, Mwigumbi Primary, Buchambi Primary, Bubiki Primary, Bunambiyu Sekondari na Ng’wanima Sekondari.


Kwa ujumla, bonanza hilo limekuwa sehemu muhimu ya kuwapa wanafunzi nafasi ya kuonesha vipaji vyao, kujenga afya ya mwili, nidhamu, ushirikiano na ushindani wa kiushindani, sambamba na kuweka msingi wa kukuza mchezo wa netiboli wilayani Kishapu kuanzia ngazi za shule.







0 تعليقات

إرسال تعليق

Post a Comment (0)

أحدث أقدم