
Mwenyekiti wa Halmasahuri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga na Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha Utawala na Mipango Mhe. Josephat Limbe akizungumza wakati wa ziara hiyo ya siku mbili kuanzia Julai 21-22, 2026
Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Josephat Limbe, kwa kushirikiana na Mbunge wa Jimbo la Kishapu, Mhe. Lucy Mayenga, imefanya ziara ya siku mbili Julai 21–22, 2026 ya kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na mtambo wa Excavator unaomilikiwa na Halmashauri.
Miradi iliyotembelewa ni pamoja na kikundi cha ufugaji wa mbuzi Mwamashele, ujenzi wa matundu sita ya choo, kichomea taka na mfumo wa maji katika Zahanati ya Ngofila, umaliziaji wa vyumba viwili vya madarasa katika Shule ya Msingi Ngunga, umaliziaji wa Zahanati ya Ikonokelo, ujenzi wa vyumba vya madarasa, nyumba za walimu na matundu ya choo katika Shule ya Msingi Bukingwamandege, kikundi cha vijana wa bodaboda Maganzo, pamoja na ujenzi wa vyumba vya madarasa na matundu ya choo katika Shule ya Msingi Bulima.
Kamati imeeleza kuridhishwa na hatua iliyofikiwa katika baadhi ya miradi huku ikitoa maelekezo kwa wataalamu na wakandarasi kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa wakati, kwa kuzingatia viwango vya ubora vilivyowekwa ili iweze kutoa huduma bora kwa wananchi.



Baadhi ya Wanafunzi wa Dalasa la Sita Shule ya Msingi Bukingwamandege wakifurahia uboreshewaji wa miundombinu ya Madalasa
Wanafunzi wa Dalasa la tatu shule ya msingi Bukingwamandege wakifurahia miundombinu bora ya kujifunzia shuleni hapo
Picha za miradi mbalimbali liyotembelewa






























إرسال تعليق